Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi (Kulia)akiwa na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema (Katikati) pamoja na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China Mhe. Li Qiang, wakiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa Ukarabati Mkubwa wa Reli ya TAZARA iliyofanyika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mulungushi Jijini Lusaka nchini Zambia. Tarehe 20 Novemba 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Prof. Makame Mbarawa kuwa Waziri wa Uchukuzi katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 18 Novemba 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. David Kihenzile kuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 18 Novemba 2025.
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Kassim Majaliwa na Rais wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye wakichanganya simenti kuashiria uwekaji wa wa jiwe la msingi wa ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge Railway – SGR) kipande cha Uvinza (Tanzania) hadi Musongati (Burundi), Lot 7&8, Tarehe 16 Agosti,2025 katika eneo la Musongati, nchini Burundi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua usafirishaji wa mizigo kwa kutumia Usafirishaji wa treni ya umeme ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma eneo la Kwala Marshalling Yard mkoani Pwani tarehe 31 Julai, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na Viongozi wa Wizara ya Uchukuzi mara baada ya kuzindua rasmi Bandari Kavu ya Kwala (Kwala Dry Port) iliyopo Kwala, Kibaha Vijijini Mkoa wa Pwani tarehe 31 Julai, 2025.
Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Serikali na Chama cha Mapinduzi mara baada ya kutembelea Bandari ya Tanga 1 Machi 2025.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi na viongozi mbalimbali wa Serikali wakikata utepe kuashiria Mapokezi ya Ndege mpya ya Serikali aina ya B787 Dreamliner mara baada ya ndege hiyo kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar mwezi agosti 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na viongozi wengine akifungua pazia kuashiria uzinduzi rasmi wa Safari za treni ya Reli ya SGR kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma 1 Agosti 2024.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile akizungumza na wananchi wa mkoa wa Tabora (hawapo pichani) katika uwanja wa Chipukizi wakati wa ziara ya Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango mkoani humo.