Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Uchukuzi

SHIRIKA LA NDEGE LA BRUSSELS KUTOKA UBELGIJI YAANDA SAFARI ZA KUJA TANZANIA

Imewekwa: 04 Jun, 2026
SHIRIKA LA NDEGE LA BRUSSELS   KUTOKA UBELGIJI   YAANDA SAFARI ZA KUJA TANZANIA

Shirika la ndege la Brussels (Brussels Airlines) kutoka Brussels nchini Ubeligiji  imeandika historia mpya Nchini Tanzania  hasa katika Sekta ya Usafiri wa  Anga, Utalii na Biashara  baada ya Shirika hilo kuzindua rasmi safari zake za mojakwamoja kati ya Brussels ,Ubelgiji kuja Tanzania kupita uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) hafla ya mapokezi yao imefanyika tarehe  Juni 3 ,2026.

Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa aliongoza viongozi mbalimbali  kuipokea ndege hiyo  amesema kuwa kuanza kwa safari hiyo ni  kufungua fursa za  kiutalii , biashara na mahusino kwa nchi mbili kati Tanzania na Ubelgiji, pia aliongeza kusema kuwa haya yote yanafanyika kutoka na mazingira mazuri yaliyotengenezwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluh Hassan.

Pia Mbarawa amesema kuwa Serikali inaendelea  kuboresha viwanja vya ndege hapa nchini hususani kiwanja cha ndege cha KIA  kwa kujenga jengo la Kisasa la Abiria ili kundelea kuvutia mashirika mengine ya ndege kuja Tanzania.

Kwa upande wake  Naibu Waziri wa  Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika  Mashariki Mhe. James Millya (Mb), amesema uzinduzi wa Safari hizo kutoka Brussels, makao makuu ya umoja wa Ulaya (EU) nia ishara ya kuimarika kwa uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya Tanzania na Ubelgiji pamoja na nchi nyingine za Ulaya.

Naye Rais wa Shirika hilo Julia Hilenbrand amesema kuwa kuanza kwa safari hizo ni hatua muhimu katika Safari za Anga kati ya Tanzania na Ubelgiji kwa  kwa sasa  watalii na wafanyabiashara watatoka Ubelgiji   na kuja Tanzania.

Huku Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka wa Viwanja vya Ndege  Abdul Mombokaleo amesema kuwa  Serikali inaendelea kuboresha  viwanja vya ndege hapa nchini ili mashirika  mengi ya ndege yaweze kuja nchini Tanzania.