Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Uchukuzi

SEKTA YA UCHUKUZI YAENDELEA KUKUZA UCHUMI WA NCHI PROF KAHYARARA.

Imewekwa: 31 Dec, 2025
SEKTA YA UCHUKUZI YAENDELEA KUKUZA UCHUMI WA NCHI PROF KAHYARARA.

Sekta ya Uchukuzi inaendelea kukuza uchumi mkubwa nchini hivyo  kupitia uchumi huo  ni muhimu kwa wadau  wote kuendelea kushirikiana na kutatua changamoto zilizopo.

Akizungumza Jijini Dar es salaam na wadau Mbalimbali  Katibu Mkuu  wizara ya uchukuzi  Profesa Godius Kahyarara amesema kuwa kupitia  kikao hiki  kimewakutanisha wadau mbalimbali nchini  wakiwemo TRA,TPA,Jeshi la Polisi, TAMISEMI, Wizara ya UchukuzI,DP World,TRC,TMA na TBS tunaenda kushirikiana kwa pamoja katika kuendeleza na kukuza uchumi wa nchi kupitia sekta ya uchukuzi.

"Aidha  kupitia Sekta ya uchukuzi tuna ,Usafiri wa Njia ya Anga, Barabara, Maji na Reli  ambapo inaleta mchango mkubwa katika uchumi wa nchi hivyo ni muhimu wadau  kuendelea kushirikiana kwa pamoja ili kufikia malengo Mahususi." Alisema Prof Kahyarara".

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Dar es salaam Abed Galus ameongeza kuwa kutokana na ongezeko  wa Meli kubwa katika Bandari ya Dar es Salaam hivyo shehena ya Mzigo umeongezeka na  kuweza kuhudumia meli kubwa zinazobeba tani  elfu sitini kwa wakati moja.

Hata hivyo  Galus amesema kuwa Mamlaka ya  bandari (TPA) kwa kushirikiana na wadau wanaendelea kuboresha miundombinu  ili  kuondoa msongamano wa malori katika eneo la Bandari hiyo.

Naye  Naibu katibu Mkuu kutoka  TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila amesema  hakuna haja ya kujenga mzani wa kupima magari katika Banadari Kavu ya Kwala hivyo magari yatumie Mzani wa Vigwaza na  kupima  katika bandari kavu ya kwala ili  kuendelea kutumia mzani wa kuhamishika.

"Katika Hatua nyingine  Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) Mhandisi Machibya Masanja amesema shirika la Reli Tanzania  (TRC )linaendelea kuboresha vichwa vya Treni ili viweze kusafairisha mizigo kutoka bandari ya Dar es salaam kuelekea bandari kavu ya Kwala  na Ihumwa Mkoani Dodoma.

Machibya amewataka  wadau kuwekeza kwenye Treni kwani sheria kwani sheria inaruhusu sekta binafsi kumiliki treni ya mizigo na abiria.